Tuesday, March 18, 2014

HATIMAYE ANDER VILLAS-BOAS KOCHA MPYA ZENIT




Zenit St Petersburg wamethibitisha uteuzi wa Andre Villas-Boas kama mbadala wa kocha Luciano Spalletti.

Kocha wa kiitaliano Spalletti alitimuliwa na klabu hiyo ya Russia wiki iliyopita baada ya kukaa kwenye timu hiyo kwa miaka mitano kufuatia mwenendo mbaya wa timu katika ligi na ulaya, baada ya kuchapwa 4-2 na Borrusia Dortmund katika mchezo wa kwanza raundi ya 16 bora.

Na Villas-Boas, ambaye amekuwa hana kazi tangu alipofukuzwa na Tottenham mwezi December mwaka jana amechukua nafasi yake kwa kusaini miaka miwili.

"Zenit wamefikia makubaliano ya mkataba wa miaka miwili na kocha Andre Villas-Boas," taarifa ya klabu ilisema.

"Mkataba utasainiwa na Villas-Boas atatambulishwa mjini St Petersburg kuwa kocha mkuu mpya wa Zenit March 20. Mkataba wa Villas-Boas unaanza March 2014 na utaendelea kwa miaka miwili." 


Kocha huyo amewahi kufundisha klabu ya fc porto ya nchini ureno, chelsea na Totenham zote za nchini england

No comments:

Post a Comment